• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC .Chacha msibani kwa aliye kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Nzega

Tarehe Iliyowekwa: February 20th, 2026

RC Chacha Aongoza waombolezaji  mazishi ya Mhe. Paschal Kigalu

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha, ameongoza madiwani, watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega pamoja na wananchi kwa ujumla katika mazishi ya mwili wa Mhe. Paschal Kigalu.


Mhe. Kigalu, aliyekuwa Diwani wa Kata ya Itilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Nzega, alifariki tarehe 17 Februari 2026 baada ya gari alilokuwa akiendesha kuhusika katika ajali iliyotokea eneo la Kitangili, karibu na stendi ya mabasi ya Nzega.


Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa, walioungana na mamia ya waombolezaji wakiwemo viongozi wa dini na wananchi wa Nzega, kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu.


Akizungumza katika mazishi hayo, Mkuu wa Mkoa Tabora alitoa pole kwa familia, ndugu na wananchi wa Nzega kwa msiba huo mzito.


“Tuwe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu na tufanye juhudi kuyaenzi mema yote aliyoyafanya marehemu katika kuwatumikia wananchi wa Kata ya Itilo na Halmashauri ya Nzega Mji kwa ujumla,” alisema.


Aliongeza kuwa mchango wa marehemu katika maendeleo ya eneo hilo utaendelea kukumbukwa, huku akihimiza umoja na mshikamano ili kuendeleza yale mema aliyoacha.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega, Bwana Shomary Mndolwa, akishirikiana na wakuu wa idara na watumishi wa umma, alisema wameendelea kuwa pamoja na familia ya marehemu katika kipindi chote cha msiba hadi mazishi yalipokamilika na mwili wa marehemu kuzikwa kwenye makazi yake ya milele.


“Hili ni pigo kubwa kwetu kama Halmashauri, na tunaomba Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi,” alisema Mkurugenzi huyo.


Mbunge wa jimbo la Nzega mjini Mhe. Hussein Bashe alihudhuria msiba huo na kumweleza Marehemu kama mpenda maendeleo na rafiki yake wa kisiasa wa muda mrefu.


Baadhi ya nyadhifa alizowahi kushika marehemu enzi za uhai wake ni pamoja na uwenyekiti wa CCM kata ya Itilo. Pia amekuwa Diwani wa kata hiyo tangu mwaka 2015 had umauti ulipomkuta.


Tarehe 5, Disemba 2025, Marehemu alichaguliwa kwa kishindo kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Nzega, nafasi aliyehudumu kwa miezi miwili na siku 12 hadi hadi tarehe 17, Februari mwaka huu

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • RC .Chacha msibani kwa aliye kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Nzega

    February 20, 2026
  • TANZIA

    February 17, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA MJI NZEGA LAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA TSH.26.1 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

    February 13, 2026
  • KAMATI YA USHAURI YA HALMASHAURI YA MJI WA NZEGA YAPITISHA BAJETI YA 2026/2027

    February 10, 2026
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017