• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mifugo na Uvuvi

Mifugo na Uvuvi ni shughuli inayofanywa na wakazi wengi wa Halmashauri ya Mji Nzega.

 Majukumu ya Idara ya Mifugo na Uvuvi/Huduma zinazopatikana katika Idara.

  • Kuwatembelea wafugaji ili kutoa ushauri wa kitaalamu katika maeneo yao ya kazi.
  • Kutoa chanjo zote za mifugo.
  • Kukagua nyama katika machinjio iliyopo katika Halmashauri ya Mji Nzega baada ya kuchinja kila siku.
  • Kutoa matibabu ya mifugo na kufanya uchunguzi wa magonjwa.
  • Ukaguzi wa afya ya mifugo na mazao yake
  • Utambuzi wa magonjwa, ufuatiliaji na utoaji wa kinga
  • Kutoa ushauri na Elimu  ya Ufugaji  bora wa mifugo
  • Kuandaa taarifa za Idara za Wiki, mwezi, robo mwaka na mwaka
  • Kufuatilia na kutekeleza miradi ya maendeleo ngazi ya kata na Halmashauri
  • Kufanya utambuzi na usajili wa mifugo na kuhuisha takwimu za mifugo
  • Kudhibiti mifugo inayoingia na kutoka ili kuepuka magonjwa ya mlipuko na migogoro kati ya wakulima na wafugaji
  • Kuunda vikundi vya wafugaji ili kuwafikishia huduma za ugani wa shughuli za mifugo kwa urahisi
  • Kupambana na kuzuia rushwa Mahala pa kazi na Nje ya kazi.
  • Kupambana na Kuzuia maambukizi  mapya ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi
  • Kusimamia, kudhibiti na kuendeleza tasnia ya uvuvi kwa jamii ya wavuvi
  • Kuratibu maendeleo ya siku kwa siku ya teknolojia ya uvuvi ili kuwa na uvuvi endelevu
  • Kusimamia raslimali za uvuvi
  • Kutoa Elimu ya ufugaji bora wa samaki.

Miundombinu ya Mifugo:
Majosho
: Halmashauri ina jumla ya majosho 7 katika Kata za Miguwa,NzegaNdogo,Itilo,NzegamjiniMashagharibi,Uchama,Mbogwe,Uchama.

Machinjio: Kwa sasa Halmashauri ina machinjio moja katika kata ya  Nzega mjini magharibi  

Minada ya Mifugo: Kuna mnada mmoja wa awali  wa Ushirika katika Kata ya Nzega Mjini  Magharibi shughuli za biashara ya mnada wa mifugo zinaendelea kwa kila siku ya jumamosi.

Mabwawa ya Kunyweshea Mifugo:Halmashauri ya Mji Nzega ina jumla ya mabwawa  saba(7)katika kata za Mwanzoli,Ijanija,Itilo,Nzega Mashariki,Mbogwe,Uchama na Nzega ndogo na mabirika matano(5)katika kata za Mbogwe,Ijanija,Uchama,Miguwa,Ijanija.

Pia Halmashauri ya mji Nzega ina miradi inayotekeleza katika Mnada wa Ushirika kama Ujenzi wa pakilio na shushio la Ng’ombe pia Ujenzi wa Vyoo vya kisasa,Banda la kuuzia nyama,Uzio katika mnada wa Ushirika.

 

Maradhi ya Mifugo:

Magonjwa ya mifugo yanayoathiri mifugo katika Halmashauri ya mji wa Nzega ni  yale yaenezwayo na Kupe kama vile Ndigana kali, Ndigana baridi,  homa ya Kizunguzungu,kokojoa Damu (Babesiosis). Vilevile kuna magonjwa ya Mlipuko kama vile ugonjwa wa miguu na midomo(foot and MouthDisease),chambavu(BlackQuarter),mapele ngozi (Lumpy skin disease),Homa ya mapafu(CBPP).Pia kwa jamii ya ndege kuna magonjwa kama kuharisha damu,kideri,Ndui na minyoo.

CHANJO YA KUZUIA MAGONJWA YA MIFUGO

Katika suala zima la kuzuia na kujikinga na magonjwa ya mlipuko, Chanjo mbalimbali za mifugo hutolewa na Idara ya Mifugo na Uvuvi ikishirikiana na wananchi husika.
Jitihada za kuzuia kuenea kwa maambukizi mapya ya magonjwa haya ambayo ni homa ya mapafu (CBPP),Chambavu(Black quarter),Miguu na Midomo(FMD)mapele ngozi(Lumpy skin),Kideri(newcastle),ndui ya kuku(Fowl pox)Kichaa cha Mbwa(rabies) zinafanyika kwa kuwahamasisha wafugaji kuchanja Mifugo yao.

Uhamilishaji wa Mifugo

Hakuna shughuli za uhamilishaji zinazofanyika kwa sasa katika halmashuri ya Mji Nzega.

UVUVI
Uvuvi ni mojawapo ya shughuli zinazofanyika katika Halmashauri ya mji wa Nzega kwa kuwa lipo bwawa la Kilimi katika Kata ya Uchama.

Shughuli za uvunaji wa mazao ya Uvuvi katika Halmashauri ya mji Nzega zinafanyika katika Bwawa la Kilimi lililoko katika kata ya Uchama , Samaki wanaopatikana ni  Aina ya sato/perege  na Kambare (Catfish).

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017