• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WANAFUNZI 1,126 WA SEKONDARI NZEGA MJINI KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE

Tarehe Iliyowekwa: October 3rd, 2025

*WANAFUNZI 1,126 WA SEKONDARI NZEGA MJINI KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2025*


Wanafunzi 1,126 kutoka shule kumi na tano (15) za sekondari zinazomilikiwa na serikali kupitia Halmashauri ya Mji wa Nzega wanatarajiwa kufanya Mtihani wa Taifa wa kumaliza Kidato cha Nne mwaka 2025.


Mtihani huo unaoendeshwa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) unatarajiwa kuanza mapema mwezi ujao na utafanyika nchi nzima kwa wakati mmoja.


Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji wa Nzega, Mwl. Leah Katamba, amesema kuwa tayari mikakati imewekwa ili kuhakikisha ufaulu wa asilimia tisini na nane (98%) kwa watahiniwa wa Halmashauri hiyo. Aliongeza kuwa lengo ni kuwa na ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Nne, huku ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Tatu ukitarajiwa kufikia asilimia sitini na tano (65%).


Mwl. Leah alitoa ufafanuzi huo katika kikao kilichowakutanisha Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule na Walimu wa masomo ya madarasa ya mtihani kwa lengo la kujadili kwa pamoja mikakati ya ushindi. Alibainisha kuwa ili kufanikisha malengo hayo, walimu wa masomo husika wanatakiwa kuongeza juhudi katika ufundishaji na kuhakikisha kuwa mada zote za mtaala zinamalizika kwa wakati.


Mikakati mingine iliyowekwa ili kuongeza ufaulu ni pamoja na kuwapa wanafunzi mazoezi na mitihani ya majaribio mara kwa mara, kudhibiti utoro wa wanafunzi na kuhamasisha utaratibu wa kujisomea nyumbani na shuleni kwa wakati wa kutosha.


Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Nzega, ambaye pia alikuwa mgeni rasmi, Bw. Shomary S. Mndolwa, aliwaasa walimu kuwa waangalifu na kuepuka vitendo vya udanganyifu wakati wa mitihani. Alisema kuwa serikali haitavumilia vitendo vya wizi wa mitihani na hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo.


“Kile tunachokitaka ni ufaulu, na tunatarajia kazi yenu njema itawezesha hilo. Lakini vitendo vyovyote vya wizi wa mitihani na udanganyifu havitavumiliwa kabisa,” alisema Bw. Mndolwa.


Kuhusu motisha kwa walimu, Bw. Mndolwa aliahidi zawadi nono kwa walimu wa shule zitakazofanikisha ufaulu mkubwa, hasa kwa shule zitakazotoa watahiniwa waliofaulu kuanzia Daraja la Kwanza hadi la Tatu bila kuwa na mwanafunzi wa Daraja la Sifuri. Alisema zawadi hizo ni pamoja na ziara ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo ndani ya nchi.


Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), mtihani wa kumaliza Kidato cha Nne mwaka 2025 unatarajiwa kuanza rasmi tarehe 10 Novemba 2025, na utahusisha wanafunzi kutoka shule za serikali na binafsi kote nchini.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MJI WA NZEGA AZUNGUMZA NA AJIRA MPYA

    October 13, 2025
  • WANAFUNZI 1,126 WA SEKONDARI NZEGA MJINI KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE

    October 03, 2025
  • TREKTA 20, POWER TILLER KULETA MAPINDUZI YA KILIMO HALMASHAURI YA MJI NZEGA

    October 02, 2025
  • SHULE SITA MPYA NDANI YA MIAKA MITANO ZA JENGWA NZEGA MJI

    September 29, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017