• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Dkt. Mpango Awasihi Wananchi wa Nzega Kujiandaa na kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Tarehe Iliyowekwa: October 9th, 2024

 JAMES KAMALA, Afisa Habari, Nzega Mji

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, amewataka wakazi wa Mji wa Nzega kujiandaa kikamilifu kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Novemba 2024. Dkt. Mpango amesema kuwa wananchi wajiandae kwa kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura ili watambulike rasmi na waweze kushiriki katika kuchagua viongozi sahihi watakaowaletea maendeleo wanayoyataka.

Dkt. Mpango alitoa wito huo siku ya Jumanne, tarehe 8 Oktoba 2024, alipokuwa akizungumza na wananchi eneo la Soko la Machinga lililopo katikati ya Mji wa Nzega. Alisimama eneo hilo kuwasalimu wananchi wakati akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Tabora, akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi.

"Niwatake wanawake hasa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa serikali za mitaa, na wapewe nafasi za kugombea ndani ya chama chetu," alisema, na kuongeza kuwa chama hicho kimekuwa kikitoa viongozi wanawake shupavu kama ilivyo kwa Rais wa sasa, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Dkt. Mpango pia amewasihi wananchi wa Nzega, pamoja na kujitokeza kujiandikisha na kupiga kura, wajilinde dhidi ya vurugu zozote ambazo zinaweza kuathiri zoezi la uchaguzi. Alisisitiza kuwa serikali iko macho na haitasita kuchukua hatua kali dhidi ya wale watakaojaribu kuhatarisha amani.

Kuhusu ujenzi wa Soko Jipya la Machinga unaotarajiwa kuanza hivi karibuni, Mhe. Makamu wa Rais aliagiza mamlaka za Wilaya ya Nzega kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanapewa kipaumbele kwenye ugawaji wa vizimba baada ya ujenzi kukamilika.

Naye Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini, Mhe. Hussein Bashe, alimweleza Mhe. Makamu wa Rais kuwa jimbo hilo linafanya vyema kwenye sekta ya elimu na kwamba wananchi wanapata maji safi na salama kutoka Ziwa Viktoria. Mhe. Bashe aliongeza kuwa miradi ya kuunganisha umeme inaendelea vizuri, na asilimia kubwa ya wakazi wa Nzega wameunganishwa na umeme majumbani mwao.

 

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WALIMU 184 AJIRA MPYA WAPATA MAFUNZO ELEKEZI

    July 09, 2025
  • KITUO CHA AFYA KITENGWE KIMEKUWA MKOMBOZI KWA WAKAZI WA KATA YA MWANZOLI NA MAENEO YA JIRANI

    July 03, 2025
  • WATUMISHI WA MJI WA NZEGA WAPATA MAFUNZO YA E-UTENDAJI

    June 27, 2025
  • MJI WA NZEGA WAPATA HATI SAFI

    June 19, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017