• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KATIBU TAWALA WA MKOA WA TABORA AKEMEA RUSHWA

Tarehe Iliyowekwa: September 1st, 2020

Katibu Tawala wa mkoa wa Tabora Ndugu Msalika R Makungu,amekemea vikali na kuwaonya wafanyakazi kwa kuwataka wasijihusishe na rushwa na kuongeza kuwa mkoa wa Tabora umejipambanua na hawatakuwa na msamaha kwa watumishi wala rushwa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora akihutubia katika kikao cha tathmini ya utendaji kazi wa halmashauri ya mji wa Nzega

Akifungua kikao cha tathmini cha utendaji kazi katika halmashauri ya mji wa Nzega kilichofanyika tarehe 01/09/2020 katika ukumbi wa KKKT NZEGA, Katibu Tawala alitoa salaam kutoka kwa Mkuu wa Mkoa kwa washiriki akiipongeza Halmashauri ya Mji wa Nzega kwa kwenda mbali zaidi katika suala la kujitathmini ili kuboresha utendaji kazi katika Halmashauri. Aliwaomba wadau wote waliohudhuria kikao hicho kutoa maoni yao bila kumumunya maneno ili lengo halisi la Serikali ambalo linaitaka kila halmashauri kujitegemea kimapato liweze kufikiwa.

Aliipongeza Serikali kuu kwa kuzijengea uwezo halmashauri zote za serikali hali iliyopelekea kuondoa unyonge wa kuwa omba omba. Alionya kuwa suala la ukwepaji kodi unaofanywa na walipa kodi lazima huwa kuwa kuna ushirikiano na watendaji wa Serikali.

Katika kikao hicho Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Nzega Ndugu Philemon Magesa aliwaomba washiriki kutoa tathmini ya utendaji kazi wa halmashauri ili kuboresha utendaji wa kazi.

Akitoa historia fupi ya halmashauri ya mji wa Nzega yenye vipao mbele vikuu vitatu ambavyo ni Mapato, Usafi wa mazingira na Utawala bora. Katika kutekeleza hayo Ndugu Magesa  alibainisha kuwa halmashauri imefanikiwa kukusanya mapato kwa asilimia 88.41% hadi sasa na kuongeza kuwa halmashauri imekuwa ikipata hati safi tangu mwaka 2015.

Hata hivyo Mkurugenzi aliweza kubainisha changamoto ambazo zinapelekea kutofikia lengo halisi la ukusanyaji mapato ambazo ni mwitikio hafifu wa wananchi juu ya suala la ulipaji wa mapato, ongezeko la watu na baadhi ya wafanyabiashara kuchelewa kulipa kodi kwa wakati.

Katika kukabiliana na changamoto hizi Ndugu Magesa alibainisha kuwa halmashauri ina mikakati ya kupambana na changamoto hizo ikiwa ni pammoja na kuhamasisha wananchi kuchangia maendeleo, kujenga vizimba vya kukusanyia taka na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

Washiriki wa kikao hicho ambao walikuwa ni wadau kutoka kada mbalimbali walipata muda wa kuchangia ambapo kwa ujumla walitoa msisitizo kwa kuiomba halmashauri kuboresha huduma zake kwa wananchi.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017