• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Naibu Waziri Mhe. Sangu Atoa Wito wa Nidhamu na Ubunifu kwa Watumishi wa Umma.

Tarehe Iliyowekwa: September 21st, 2024

Na James Kamala, Afisa Habari, Halmashauri ya Mji Nzega.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Clement Sangu amewataka watumishi wa umma kuwa wabunifu na kufanya kazi kwa bidii katika kuwahudumia wananchi ili kuleta tija kwa maendeleo ya taifa. Aidha, Mhe. Naibu Waziri huyo amewataka waajiri wote katika utumishi wa umma kuhakikisha wanafanya kazi kwa karibu na watumishi ili kuepusha migogoro isiyo na tija kwenye utumishi wa umma.

Aliyasema hayo siku ya Ijumaa ya tarehe 20/09/2024 aliposikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani Tabora. “Watumishi wa umma mnapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia nidhamu, ubunifu, kuboresha na kutathmini utendaji wenu ili wananchi waweze kupata matokeo chanya kwenye huduma wanazopatiwa,” alisema Mhe. Sangu.

Aliongeza kuwa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ikitenga na kutuma fedha za miradi ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali kama vile afya, elimu na miundombinu, na hivyo ni wakati sasa wa watumishi wa umma kuhakikisha wanakuwa na utendaji unaoendana na kasi hiyo.

Kwa upande wa upungufu wa watumishi katika Halmashauri ya Mji wa Nzega na Mkoa wa Tabora kwa ujumla, Mhe. Sangu alisema tatizo hilo tayari limepatiwa ufumbuzi kwani mchakato wa kuajiri watumishi wa kuziba upungufu huo tayari umeanza. “Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa vibali vya ajira mpya zaidi ya elfu arobaini na saba (47,000), na tayari Mkoa wa Tabora unatarajia kupata watumishi wapya zaidi ya elfu nne (4,000), tukianza na kada za afya,” alieleza Mhe. Sangu.

Kuhusu upandishaji wa vyeo kwa watumishi wa umma, Naibu Waziri huyo alisema kuwa serikali imekwisha tenga fedha za kutosha kwa ajili ya mchakato huo, ikiwemo pia fedha za kulipa madeni mbalimbali  kama vile malimbikizo ya mishahara ya watumishi.

 Wakati huohuo, Mhe. Sangu aliwaasa waajiri kuhakikisha wanatoa mafunzo ya awali kazini kwa watumishi wapya ili waweze kujua wajibu wao na haki zao, na hivyo kuepusha migogoro kazini na mashauri ya kinidhamu katika maeneo ya kazi.

“Wajulisheni na kuwaelekeza mazingira ya kazi, kanuni, na sheria za utumishi wa umma ili waweze kufanya kazi kwa uhuru na amani yenye tija kwa utendaji uliotukuka,” alisisitiza Mhe. Sangu.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Ricardo Katambi Komanya, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega, Bi. Leah Kibaki, na watumishi kutoka Idara na Vitengo mbalimbali katika Halmashauri hiyo.

Mwisho.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017