• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TASAF ILIVYOKWAMUA UCHUMI WA KAYA MASIKINI HALMASHAURI YA NZEGA MJI

Tarehe Iliyowekwa: December 5th, 2022

TASAF ILIVYOKWAMUA UCHUMI WA KAYA MASKINI HALMASHAURI YA MJI NZEGA

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) unaotekeleza Mpango wa Kunusuru kaya Maskini  umekua chachu ya ukuaji wa uchumi kwa walengwa wa Mpango huu ambapo kwa Halmashauri ya Mji wa Nzega imekwisha pokea kiasi cha Tsh 716,782,351.00 kwa kipindi cha Julai 2020 hadi Julai 2022 ambacho kimenufaisha  kaya 1,733.

Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji wa Nzega Bw.Denis Kazinja  Anasema,”TASAF imewezesha walengwa  kujikita katika shughuli za uzalishaji mali kama vile kilimo,ufugaji na biashara ndogo ndogo na mahitaji mengine ya kijamii hali inayobadilisha uchumi wao kwa kuanza kujiingizia vipato ambavyo vinawawezesha kukidhi mahitaji yao ya kila siku”.

Mmoja kati ya wanufaika hao, Bi. Consolata Michael(47) mama wa watoto wawili na mjukuu mmoja anayeishi na mume wake mtaa wa Utemini kata ya Nzega mjini Magharibi. Mama huyu kabla ya kujiunga na TASAF aliishi katika nyumba yenye kuta za  maturubai ambapo hakuwa na chanzo cha uhakika cha kujiingizia kipato wala hakuweza kupata milo mitatu kwa siku. Baada ya kusajiliwa TASAF kwa sasa ameweza kuanza kujenga nyumba na kununua mbuzi na kuwafuga kwa kuwekeza kidogo kidogo. “nilianza kupokea ruzuku mwaka 2015 malipo yangu ya  kwanza na ya pili niliyatumia kwa mahitaji ya nyumbani,walipaji kutoka TASAF walikua wakitoa elimu kuhusu umuhimu wa kuweka akiba kidogo kidogo ndipo nilipoamua kufanya hivyo na hivi sasa najionea matunda” alisema Consolata

Naye Simion Ntemanya(50) Baba wa watoto wanne anayeishi na familia ya watu sita ambaye kupitia mpango huu ameweza kuanzisha biashara ya magodoro ya pamba anasema “nilianza kutengezeza godoro moja na kuliuza sh. 6000 hadi sh.7000 na kupata faida ya Sh.3000 hadi 4000 kwa godoro moja, sasa naweza kutengeneza magodoro manne kwa mwezi  hivyo faida imeongezeka.shughuli hii naifanya wakati wa kiangazi msimu wa kilimo siwezi kuifanya kwani nakuwa shambani kwa ajili ya kilimo”

Akizungumza, Bi. Rejina kulwa (50),mkazi wa kijiji cha kitangiri ambaye ni mama watoto sita mnufaika wa mpango wa TASAF yeye aliweza kununua kuku watano hadi kufikisha kuku 40 “Kuku walipofika 40 niliwauza na kununua mbuzi wawili jike ambao hadi kufikia mwaka 2018 nilikua na mbuzi 30 nikawauza mbuzi wote  na kununua ardhi”alisema Bi.Rejina

Baada ya kununua ardhi aliweza kupanda mbegu ya mpunga na kuvuna magunia 30 na kuyauza alipata kiasi cha sh.1,600,000/=. Bi.Rejina aliamua kununua ng’ombe wadogo saba na kuwafuga kwa muda wa mwaka mmoja na baadaye mwaka 2019 aliwauza ng’ombe wanne na kununua ng’ombe mmoja mwenye nguvu ili kupata ngombe wa kulimia shamba.

Bi.Rejina ameendelea kufanya shughuli za kilimo na kufanikiwa kujenga nyumba yake ambapo sasa anaishi na watoto wake sita.

Bw. Denis Kazinja  anawashauri Walengwa  kuendelea kuwekeza katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali kwa kutumia ruzuku wanazoendelea kupata ili ifikapo mwisho wa mradi huu wawe wamekwisha kuwa na uwezo wa kujitegemea.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017