• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

UZINDUZI WA MIONGOZO YA ELIMU KWA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI

Tarehe Iliyowekwa: September 28th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Nzega ACP.ADVERA BULIMBA, tarehe 28.09.2022 katika ukumbi wa SERENE ulioko katika Halmashauri ya mji Nzega amezindua Mwongozo wa elimu kwa shule za Msingi na Sekondari.Miongozo hiyo iko mitatu na imezndiliwa kitaifa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.wadau mbalimbali waliohudhuria kikao ni pamoja na madiwani,maafisa kata,vijiji na mitaa,maafisa Elimu Kata,Wakuu wa Idara na Vitengo,wadhibiti obora elimu,Afisa Tarafa,wakuu wa shule za msingi na sekondari pamoja na wazee maarufu.

Akiongea na wadau hao wa elimu Mkuu wa Wilaya,alisema kuwa ukiona mkakati wa elimu unazindiliwa ujue kuna changamoto zinazojitokeza na kwamba kila mmoja atapimwa kulingana na utekelezaji wa miongozo hiyo.

Amewataka wadau hao kuhakikisha kuwa swala la kushuka kwa elimu halitatokea tena katika Wilaya yake.

Amewataka maafisa elimu kata kuwajibika na kama hawawezi ahame mwenyewe kabla ya yeye kuchuka hatua.Amewata pia kuhakikisha wanaiarisha ufuatiliaji wa elimu hasa utoro mashuleni.

Amesisitiza nidhamu ikawe msingi wa kazi

Ametaka elimu ikawe ajenda ya kudumu katika vikoa katika ngazi zote za Wilaya.

“Simamieni miongozo ya uteuzi kwa haki (nyie maafisa elimu) kama mtu hana sifa msimteue” Alisema Mkuu wa Wilaya.

Amewasititiza wazazi wanaokwamisha mikakati ye elimu wachukuliwe hatua.amesema hayo kupitia kwa wazee maarufu waiohudhuria kikao hicho akiwemo Marry Igogo.

Ameiopongeza Halmashauri ya mji Nzega kwa ufaulu wa jumla kuanzia darasa la nne,la saba,form two, form iv na form six kwa ufaulu wa asilimia mia moja.

Mkuu wa Wilaya ameahidi kutolala hadi hali ya elimu iimarike.

Amehoji pia kama fedha zinazotolewa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mh.Samia Hassan Suluhu zina tatua changamoto za kielimu hasa miundombinu ya shule ,madawati na chakula.

Amewataka viongozi wa kuhakikisha wanatatua kero za walimu hasa stahiki zao zilipwe kwa wakati ili kuwaondolea usumbufu.

“Kila mwanafunzi mwenye umri wa kwenda shule aandikishwe na kuhakikisha wanakwenda shule.Kazi hii wasimamie watendaji wakishirikiana Maafisa Elimu Kata” Alisema Mkuu wa Wilaya.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Nzega Ndugu. Shomary S. Mndolwa katika kikao hicho cha ufunguzi wa Miongozo ya Elimu kwa shule za msingi na secondary alisema kuwa Halmshauri imepokea fedha kutoka kwaajili ya uimarishaji wa elimu hasa katika eneo la miundo mbinu. “Halmshauri imetenga pia fedha kiasi cha millioni 480 kutoka mapato ya ndani kwaajili ya uboreshaji wa miundombinu ya Elimu”.Alisema Mkurugenzi

Amesema kuwa ili kuinua kiwango cha ufaulu katika Halmashauri  atatoa motisha kwa shule zitakazo fanya vizuri.”Nataka kuahidi, shule itakayoongoza kwa ufaulu itapewa shilingi milioni moja (1,000,000) na Mwalimu Mkuu atapewa shilingi laki tano (500,000)”Alisema Mkurugenzi

AFISA ELIMU SEKONDARI BI.LULU B NCHIHA  Akisoma taarifa yake mbele ya mgeni Rasmi alisema kuwa Ofisi ya Rais TAMISEMI imekuwa ikifanya ufuatiliaji na tathmini ya mara kwa mara ili kuona maendeleo ya Elimu ya Msingi na Sekondari.  Tathmini ya hivi karibuni imebaini uwepo wa mafanikio na changamoto kadhaa ambazo kwa pamoja zimesababishwa na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika Sekta hii. Ili kukabiliana na changamoto zinazoikabili Sekta hii na hivyo kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondari Nchini, Serikali imeandaa miongozo mitatu za kuzingatiwa katika usimamizi na uendeshaji wa shule:-

  • Mwangozo wa Uboreshaji Elimu Msingi na Sekondari: Nini kifanyike?
  • Mwongozo wa Mkakati wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji ngazi ya Elimu msingi.
  • Mwongozo wa Uteuzi wa Viongozi wa Elimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mikoa.

LENGO LA MWONGOZO NA MKAKATI WA KUIMARISHA UFUNDISHAJI KATIKA NGAZI YA ELIMU MSINGI NA SEKONDARI

  •  
  • Miongozo hii  iliyoandaliwa Kitaifa, inalenga yafuatayo:
  • Kubainisha mafanikio ya Sekta hii nchini
  • Kubainisha changamoto zinazoikabili Sekta hii katika ngazi na nyanja mbalimbali.
  • Kubainisha hatua za kuchukuwa ili kukabiliana na changamoto zilizobainishwa ili kuboresha elimu ya Msingi na Sekondari Nchini.
  • Kuweka Dira ya kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa Elimu Msingi na Sekondari wenye tija. 
  • Kuimarisha Usimamizi na Uendeshaji kwa njia ya kuimarisha Uongozi katika ngazi mbalimbali.
  • Kuliwezesha Taifa kufikia malengo ya Elimu ya Msingi na Sekondari kama yalivyobainishwa kwenye Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 na Miongozo mingine ya Kitaifa ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 na Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025.

AFIS ELIMU MSINGI NDG.AJALII M MARUMWENGU alitoa ufafanuzi juu ya miongozo hiyo kuwa ni maagizo ya Serikali na lazima yatekelezwe kwa ufanisi.Alisema kuwa miongozi hiyo ilizinduliwa Kimkoa tarehe 16/08/2022 wakati wa umitashumta.

WADAU WA ELIMU

Mzee maarufu, MZEE SAMOTA alisema kuwa atachangia baiskeli mia moja(100) kwa shule ambayo itaingia kumi bora katika Mkoa wa Tabora..hii ni katika harakati za kuinua kiwango cha Elimu katika Wilaya ya Nzega

Naye Mzee maarufu Mama Merry Igogo wakati akichangia alimwomba Mzee Samota kuwa mfadhili wa Walimu Wakuu.Alimwomba awafadhili Mabati ili waweze kujenga na kuishi katika mazingira mazuri ambayo yatawawezesha kufanya kazi vizuri.

Madiwani pamoja na wajumbe wengine waliokuwepo kwenye kikao hicho walichangia juu ya uimarishaji na uboreshaji wa elimu ikiwa ni pamoja na wazo la kuwa na mfuko wa Elimu wa Wilaya.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017