• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI HALMASHAURI YA MJI NZEGA KUBURUZWA MAHAKAMANI

Tarehe Iliyowekwa: July 2nd, 2018

Halmashauri ya Mji Nzega imetoa siku tatu kwa wazazi wenye watoto watoro kuhakikisha watoto hao wanarudi shuleni ili kuepuka hatua Kali za kisheria zitakazo chukuliwa dhidi yao.

Wito huo umetolewa leo na Onesmo Kisoka Katibu Tawala wa Wilaya ya Nzega kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya  wakati akipokea maandamano ya kupinga utoro na kuhamasisha mahudhurio shuleni kwa kuzindua kauli mbiu ya "opareshen ya kamata weka ndani kwa kutotii amri halali" ambapo amesema kuwa kufuatia opareshen hiyo wanatoa msamaha kwa muda wa siku tatu kwa wazazi watakao chukua hatua ya kuwarudisha watoto wao shule na baada ya siku hizo kuisha watafanya msako nyumba kwa Nyumba na kuhakikisha wote wenye watoto watoro wanakamtwa na kufikishwa mahakamani.

Bwana Kisoka amefafanua kuwa wana orodha ya watoto wote watoro na wanachotakiwa kufanya ni kuwafuatilia na kuwafikisha wazazi wao kwenye vyombo vya sheria Ili watoto hao waweze kurudi shuleni na kupata haki ya kupata elimu ili waweze kuondokana na umasikini, ujinga na maradhi kwani elimu ni ufunguo wa maisha.

Alieleza kuwa katika halmashauri zote Mbili Halmashauri ya wilaya na ya Mji jumla ya wanafunzi mia 432 wa sekondari na wanafunzi elfu 1078 wa shule za msingi ni watoro ambapo amezitaka halmashauri  kwa kushirikiana na serikali za vijiji kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni kwani kutokuwa na utaratibu huo kunadumaza maendeleo ya elimu na kuchochea utoro kwa wanafunzi.

Aidha akisoma taarifa,  Mratibu wa maandamano hayo katika Halmashauri ya Mji, Bwana Hamdan Shemzigwa amesema kuwa halmashauri ya Mji ambayo ni mojawapi kati ya Halmashauri 8 za Mkoa wa Tabora na una jumla ya kata 10 ambapo una shule za msingi 34 zenye jumla ya wanafunzi elfu 21,813 wavulana wakiwa ni elfu 10,710 na wasichana elfu 11,103 na walimu  456 huku sekondari zikiwa 11 zenye wanafunzi elfu 4,557 wasichana 2,031 pamoja na wavulana 2,536 na jumla ya walimu mia 123.

Shemzigwa akisoma taarifa,  aliema kuwa maandamano hayo yana lengo la kupinga utoro na kuhamasisha mahudhurio shuleni kwani utoro unaadhiri maendeleo ya Mtoto kitaaluma na kushindwa kufikia malendo ya watoto kupata elimu bora .

Ameeleza utoro kwa mji wa Nzega kwa shule za msingi ni jumla ya wanafunzi 91, wavulana wakiwa 44 na wasichana 47 na shule za sekondari jumla ni 112, wavulana 76 na wasichana 36 ambapo Mikakati iliyofanyika ni kuwabaini watoto kimadarasa na kwa majina ili kuweza kuwafuatilia wazazi na kuwachukulia hatua za kisheria na katika suala la mimba katika mji wetu kuna mimba 9,  nne (4) zikiwa za shule za msingi na tano(5) zikiwa shule za sekondari ambapo zote zimeripotiwa katika vyombo vya sheria na kesi zinaendea kusikilizwa" Alisema

Alifafanua kuwa katika kuhakikisha Mtoto anafikia malengo yake kwa kumuepusha na vitendo kandamizi kila mwananchi anapaswa kutambua wajibu wake katika Jamii ambapo amewataka wazazi na walezi kufuatili mahudhurio ya watoto na kuhakikisha wanakagua maendeleo yao kitaaluma, kuwalea watoto wao katika maadili mema yanayokubalika na jamii, kuzungumza na watoto wao katika hatua mbalimbali za makuzi kupunguza na kudhibiti mihemko, kuwapatia watoto wao mahitaji muhimu kama vile chakula na mavazi ili kuwaepusha na vishawishi na hatimaye mimba za utotoni.

Bwana Shemzigwa akisoma taarifa hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Idara ya Elimu Msing ametoa wito kwa Jamii kuzingatia sheria ya elimu namba 25 ya mwaka 1978 inayomtaka kila mwanafunzi aliyeandikishwa shule kuhudhuria masomo hadi atakapomaliza hivyo ni jukumu la kila mwananchi kusimamia hilo pamoja na kujiepusha na vitendo vya kumkandamiza Mtoto ili watoto waweze kufikia ndoto zao .

Pia ameiomba serikali kutimiza wajibu wake kwa kusimamia vizuri kanuni, Sera na miongozo dhidi ya vitendo hivyo kwa kuhakikisha wahusika wanawajibishwa ikiwa ni pamoja na kuendelea kuboresha miundo mbinu ya shule na kutatua changamoto ya upungufu wa walimu .

Sambamba na hayo pia ameishukuru serikali ya awamu ya tana kwa kuleta elimu bure, kuboresha miundo mbinu, kugawa vifaa vya kujifunzia na kufundishia pamoja na vifaa vya maabara kwa kupitia Sera ya elimu bila malipo..

Awali akimkaribisha Katibu Tawala wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Mji alisema,  maandamano hayo yamelenga kupinga ajira na utumikishwaji wa watoto katika kazi za majumbani, migodini, mashambani, kumbi za starehe, vilabu vya pombe, kuchungishwa ng'ombe pamoja na kupinga ukatili wa kijinsia na mimba za utotoni.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017