• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI WA KILIMO NA MBUNGE WA JIMBO LA NZEGA MJINI AKAGUA MIRADI JIMBONI KWAKE

Tarehe Iliyowekwa: October 18th, 2022

Waziri wa kilimo na mbunge wa jimbo la nzega mjini amefanya ziara ya kukagua miradi katika jimbo lake la nzega Mjini.

Katika ziara yake aliyoifanya tarehe 18/10/2022 ametembelea jumla ya miradi mitatu 3 ambayo ni

  • Ujenzi wa shule ya msingi katika mtaa wa utemini kata ya Nzega Mjini Magharibi
  • Ujenzi wa shimo (ponds) ya maji taka katika kijiji cha Uchama kata ya Uchama.
  • Ukarabati wa bwawa la iduduo katika kijiji cha Idudumo kata ya Mwanzoli

Akiwa katika mtaa wa Utemeni kutembelea ujenzi wa shule ya msingi alimshukuru Mh. Rais Samia Hassan Suluhu kwa kutoa tshs milioni 200 (200,000,000) kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo.Amesema shule hiyo ni muhimu kwani itawasaidia watoto waliokuwa wanaenda/kutembea  umbali mrefu kupata elimu.Shule itakuwa na madarasa 9 pamoja na matundu ya vyoo

Amewashukuru wananchi wa mtaa huo kwa kukubali kutoa eneo la ujenzi wa shule na kulipwa fidia yenye jumla ya tshs 9,000,000 (milioni tisa).Amewashukuru pia kwa kujitolea kuchimba msingi kama nguvu kazi kutoka kwa jamii.Amewataka kuendelea na moyo huo wa kupenda elimu na kuwataka jamii nyingine Nzega kuigs mfano huo.

Akiongea na wananchi wa mtaa huo Mh.Bashe aliongeza kuwa kuna mkakati wa kuwawezeshs wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne kufanya vizuri katika mitihani yao.Mkakati huo ni wa kuanzisha kempu (camp) katika shule ya Sekondari Bulunde ambapo kuna jumla ya walimu 20.Amewataka wazazi kutokuwa kikwazo cha cha kutowaruhusu wanafunzi kwenda camp.

Mh.Bashe amesema kuwa ili kukabiliana na upungufu wa chakula Serikali imetoa mahindi ambayo yatauzwa kwa tshs 750/= kwa kilo.

Amewataka wananchi wa Nzega kujiandiksha katika mfumo wa kielektronic  kwaajili ya kupata mbolea ya ruzuku.amesisistiza kuwa yeye kama Mbunge  atanunua mbegu ambayo itagawiwa kwa wananchi bure.mbegu hizo ni:

  • Mahindi
  • Alizeti
  • Mihogo

Amewataka Wananchi kuhakikisha wanatumia mvua za kwanza kwaajili ya kilimo.

Mh.Bashe ametaja aina nyingine za  miradi ambayo inatekelezwa katika jimbo lake  na hatua mbalimbali zilizofikiwa kama ifuatavyo:

  • Mradi wa taa za barabarani ambao unaoendelea katika mitaa ya Mji wa Nzega ambapo umeshasimikwa katika eneo la Mjini.
  • Ujenzi wa stand mpya ambapo mkandarasi yuko site
  • Maborsho wa soko la kachoma ambapo bado kuanza
  • Uboreshaji wa eneo la wamachinga (parking)

Akiwa katika Kata ya Uchama katika kijiji cha Uchama Mh.Bashe ametembelea mradi wa ujenzi wa shimo la maji taka ambapo Meneja wa Mamlaka ya Maji Mjini(NZUWASA)  Eng.Kilundumya amemweleza mbuge kuwa mradi huo umefikia 90% ya utekelezaji.Amesema kuwa Halmashauri ya Mji Nzega itakuwa ni Halmashauri ya pili kuwa na mradi huo baada ya Kahama.

Akizungumza na wananchi wa Uchama Mh.Bashe  amemshukuru Mh.Rais kwa kutoa fedha kwaajili ya ujenzi wa mradi huo.Amewataka wananchi hao kutosikiliza longolongo badala yake waulinde mradi huo kwani una faida mbalimbali ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa mbolea. 

Akiwa katika kata ya Mwanzoli, kijiji cha idudumo Mh.Bashe ametembelea mradi wa ukarabati wa ujenzi wa bwawa la IDUDUMO  na kujionea shughuli zinazofanyika ikiwa ni pamoja na

  • Kuongeza  kimo cha ukuta
  • Kutengeneza mifereji ya kupeleka maji mashambani
  • Ujenzi wa utoro wa maji(spillways).

Alimtaka mkandarasi kufanya yafuatayo;

  • Wafanye extension hadi iduguta,tembezi na mboga
  • Wafanye design ya phase 3
  • Kuweka mipaka katika eneo la bwawa kuepuka kuvamiwa
  • Kutoa matoleo kwaajili ya kunywesha mifugo

Akiongea na wananchi wa Kijiji cha Idudumo amewahakikishia kuwa ahadi zote alizowaahidi kipindi cha kampeni atazitekeleza zote ikiwepo ahadi ya maji ambapo alimtaka Meneja wa Maji NZUWASA kuhakikisha kabla ya mwezi 12 mwaka 2022 maji yawe yameshafika katika kijiji hicho.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017