ALAT MKOA WA TABORA YA PATA MWENYEKITI
Jumuiya ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Tabora imefanya uchaguzi wa viongozi mbali mbali akiwemo mwenyekiti wa jumuiya hiyo ,tukio hilo limefanyika leo kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Mji Nzega uliopo eneo la Ipazi.
Ambapo katika nafasi ya mwenyekiti wagombea walikuwa wawili ambao ni Pasikali Kigalu mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Nzega pamoja na Gulam Hussein Meya wa Manispaa ya Tabora
Wajumbe walio piga kura walikuwa 28 ambapo Gulam Hussein alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Tabora.
NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)
Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA
Simu ya Mezani: +255677003373
Simu ya Mkononi: +255677003373
Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz
Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017