• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
NZEGA TOWN COUNCIL
NZEGA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Nzega

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Origin
      • Ukubwa wa Eneo
      • Watu wa Eneo Husika
      • Hali ya Hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
      • Orodha ya Madiwani
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji, Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Takwimu, Usimamizi na Ufuatiliji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio Vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma Mbalimbali
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha wa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kukutana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA MJI NZEGA YAVUKA LENGO KWA UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI KWA MWAKA WA FEDHA 2017/2018

Tarehe Iliyowekwa: August 2nd, 2018

HALMASHAURI ya Mji wa Nzega imefanikiwa kuvuka lengo la utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kutokana na mapato yake ya ndani kwa vikundi vya vijana na wanawake ilivyoyokuwa imekusudia ambapo imetoa milioni 161.6 ambayo ni sawa asilimia 104.5 katika mwaka wa fedha uliopita.

Hatua hiyo inatokana na Halmashauri  kuwa imepanga kutoa mikopo kwa vikundi hivyo ya milioni 154.6 lakini ikafanikiwa kuvuka lengo.

Kauli hiyo ilitolewa  na Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Mji wa Nzega Philemon Magesa wakati Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika tarehe 31.07.2018

Alisema tumefanikwa kukopesha kupitia SACCOS milioni 116 kwa vikundi 67 vya wanawake na milioni 45.9 kwa vikundi 9 vya vijana.

Aidha Magesa alisema kuwa hadi kufika mwezi Juni mwaka huu jumla ya milioni 87.4 kati ya milioni 182.9 sawa na asilimia 47.8 zilikuwa zimerejeshwa na vikundi vya wanawake na vijana vilivyokopa.

Alisema kuwa baadhi ya vijana wamekuwa wagumu kurejesha mikopo ukilinganisha na wanawake ambao wengi wao wamekuwa waaminifu na warejesha vizuri  mikopo.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Nzega Godfrey Ngupula aliitaka Halmashauri  kuwa makini katika utoaji wa mikopo kwa vikundi ili kuepuka upoteaji wa fedha hizo na kuzifanya zizungeke na ziwafikie vijana , wanawake na watu wenye ulemavu wengi kwa ajili ya kujiendeleza.

Alisema ni vema kutoa mikopo kwa vikundi ambavyo bado vinadaiwa na kuongeza ni vema wakopaji wakaelimishwa kuwa fedha hizo ni mkopo na sio ruzuku ili wawe na wajibu wa kuzitumia kwa makusudi wakiokopea na sio kufanya starehe.

Katika hatua nyingine Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Nzega limemchagua kwa kura zote Diwani wa Kata ya Mbogwe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Kapaya Sozy kuendelea kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kipindi cha pili mfulululizo.

Diwani huyo alipata kura zote 14 zilizopigwa na Madiwani za Madawani waliohudhuria Baraza hilo huku Diwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo naye akimuunga mkono mgombea pekee huyo.

Awali Mkurugenzi Mtendaji Magesa alisema kila mwaka wa fedha unapoisha wanalazimika kuchagua Makamu wa Mwenyekiti na ndipo walipoviandikia Vyama vya CCM na CHADEMA kuleta mapendekezo ya majina ya Madiwani ambao wangegombea nafasi hiyo lakini ni Chama cha Mapinduzi ndio kilijibu kwa kumpendekeza Diwani wa Kata ya Mbongwe kuendelea kutetea nafasi hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri William Jomanga alisema kuchaguliwa kwa kura zote kwa Diwani huyo kumeonyesha kuwa Madiwani wenzake wanayo imani kubwa kwake ya kutaka aendelea kumsaidia katika kuliongoza Baraza hilo.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 17, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA October 01, 2019
  • KOROSHO- ZAO LA KIMKAKATI July 23, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA December 16, 2022
  • Onesha Yote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA INEC WAASWA KUWA WAADILIFU

    April 29, 2025
  • MKURUGENZI WA MJI WA NZEGA ANAWATAKIA WATUMISHI WOTE NA WAKAZI WA MJI WA NZEGA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA

    April 20, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA PATA MAFUNZO YA MFUMO WA IFT-MIS

    April 17, 2025
  • MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA IRANI ASILIMIA 100%

    April 16, 2025
  • Onesha Yote

Video

JARIDA KITUO CHA AFYA ZOGOLO & BULUNDE SEKONDARI
Video Nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Matukio
  • Matangazo
  • Zabuni

Kurasa zinazofanana

  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tabora RS
  • TAMISEMI
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    NZEGA TOWN COUNCIL (HALMASHAURI YA MJI NZEGA)

    Sanduku la Barua: S.L.P 256 NZEGA-TABORA

    Simu ya Mezani: +255677003373

    Simu ya Mkononi: +255677003373

    Barua Pepe: td@nzegatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki zote zimehifadhiwa na nzegatc 2017